MWANAJESHI AMKATALIA TRUMP soma zaidi hapa

Robert Harward
                   Robert Harward, 60, ni mwanajeshi wa zamani wa jeshi la majini la Marekani
  • Robert Harward, 60, ni mwanajeshi wa zamani wa jeshi la majini la Marekani
Mwanajeshi wa zamani aliyekuwa amependekezwa na Rais wa Marekani Donald Trump kuwa mshauri wake wa masuala ya usalama wa taifa amekataa kazi hiyo.
  1. Robert Harward alitarajiwa na wengi kuchukua wadhifa huo ulioachwa na Michael Flynn aliyefutwa kazi na Bw Trump Jumatatu.
Afisa mmoja wa ikulu ya White House alisema sababu ya Bw Harward kukataa nafasi hizo ni kwamba ana majukumu mengi ya kifamilia na kifedha.
Bw Flynn alimpotosha makamu wa rais Mike Pence kuhusu mazungumzo yake na balozi wa Urusi nchini Marekani ambayo aliyafanya kabla yake kuteuliwa rasmi kuwa mashauri.
  • Pigo hilo kwa Bw Trump, la kukataliwa kwa uteuzi wake na Harward, lilitokea saa chache baada ya Bw Trump kupuuzilia mbali ripoti kwamba utawala wake umekumbwa na mtafaruku mkubwa.

Comments